Pages

Friday, 13 June 2014

NDOA TAJIRI KUPITA ZOTE ZILIZOWAHI KUFUNGWA

NAMSHUKURU MUNGU KWA AJILI YA SIKU YA LEO NINAPENDA KUWEKA MASOMO HAYA YA PEKEE KUTOKA KWA PASTOR MWANGA AMBAYO MIMI BINAFSI YAMENIBARIKI SANA.UBARIKIWE UNAOENDELEA KUWAALIKA WENZAKO WASOME



NDOA TAJIRI KUPITA ZOTE ZILIZOWAHI KUFUNGWA  

 Mungu Mwana – YESU KRISTO ndiye aliyeanza kufunga ndoa ya kwanza. Ndoa iliasisiwa kwa njia ya muujiza wa ajabu! Wakati Yesu alipomuoperate Eva. Hata bado Yesu alionyesha heshima ya ndoa kwa kuhudhuria karamu ya harusi. Ajabu ya Hakika – muujiza wa kwanza tena kwa mwanadamu aliofanya Yesu alianzia pale Kana ya Galilaya kwa kugeuza maji kuwa divai. YOHANA 2:1-5. Ndoa ya fahari na tajiri ambayo imeshawahi kufungwa ni ile ya kana ya Galilaya ilifanikiwa kumwalika Yesu. Na wala sio Clinton bali mfalme wa wafalme. Hawakupungikiwa chochote. Hata ijapokuwa maarusi walikuwa maskini lakini kwa kuhudhuria Yesu – tajiri mkuu ilikuwa tajiri kupita zote.
-          Kwanini Yesu alifanya miujiza katika matukio haya ya ndoa? Ndoa ilikwisha poteza thamani yake kama alivyoasisi. Heshima, upendo, furaha, utii, n.k. vilitoweka ndani ya ndoa na kilichobaki unyama, mauaji, chuki, magomvi, n.k. Mwanaume kumkata mapanga mkewe bila hofu.
-          Fundisho la Yesu pale Kana ya Galilaya ni kuwa ndoa na Yesu havitenganishiki. Anapoingia ubia maisha yanakuwa matamu kama divai iliyochujwa sana katika urojourojo wake tena ni mbaraka. Pale Edeni alifanya muujiza akijua ndoa itaingia shidani, mponyaji wa kweli wa ndoa sio mahakama wala wazazi au marafiki wala vikao vya kata. Hivyo ndoa na Yesu ni amani, furaha, na pia bubujiko la maji ya uzima.
Kicheko cha furaha kinaletwa na kitu kinachoitwa UPENDO WA KRISTO. Kabla sijazungumzia neno upendo hebu tuelewe maana ya ndoa: EBRANIA 13:4 – Malazi yawe safi? Iheshimiwe na watu wote? Kwanini Mungu atamke maneno kama hayo?
Neno ndoa ni ‘marriage’ means BED. Kiswahili ni kitanda. Mchungaji anapofungisha ndoa inamaanisha anatoa ruhusa ya kwenda kulala pamoja sio kama kaka na dada bali kufurahi mbaraka wa ndoa yaani tendo la ndoa. KISA CHA CHIBILA.  Hivyo mnapoolewa wana wa kike usifikiri mnaenda kuosha vyombo na kufua au kupika – acha! ILI NDOA IITWE NDOA NI MPAKA IWE NA UTAKATIFU WAKE KITANDANI.
-          Sio kanisa au serikali inayoweza kuita ndoa mahali ambapo match imefanyika na tena watu wamekula lakini hakuna kilichotendeka, moja kwa moja hiyo sio ndoa kisheria na kimbingu.
Biblia inaposema malazi yawe safi  - sio swala la usafi wa mashuka bali ina maana lazima kila mmoja awe mwaminifu kwa mwenzake – unapozini maana yake umeoa au umeolewa na mtu zaidi ya mmoja. Hili ndilo YESU anasema mwaweza kutengana tu kwa uasherati – uasherati maana yake uchafu. Mnapotoka nje ya ndoa hapo umechafua kitanda yaani ndoa yako. MITHALI 7:9-23. ; 6:26-29,32-33.
Biblia inaposema ndoa iheshimiwe ina maana kila mmoja ajali wajibu wake. Mume upendo na mke utii. Pia tambua unapooa mnaacha wapenzi wote na pia na wachumba wote kisha wazazi au mashemeji au mawifi hawana ubia hapo tena. Jihadhari usioe mke wa ukoo. Baba mkwe lazima aiheshimu ndoa yako sio apange masharti yake- hiyo ni serikali nyingine tayari.
ZINGATIA UPENDO – Upendo wa kweli haujengwi na fedha, nyumba, fedha, au mali bali YESU – IBADA. YESU AWE MFALME  - ASUBUHI, MCHANA NA JIONI. KISHA MUME AWE KIONGOZI TU SIO MTAWALA NA MKE AWE RAIA MWEMA.
Upendo sio kumuona mwenzako haendi kanisani na wewe unanyamazia .


Philosopher mmoja anayeitwa PLATO: Anasema ndoa ni kama ngazi yenye hatua za kupanda. Hatua ya kwanza ni kifungo cha UPENDO.
-          Hapa lazima umwambie mwenzako ulichompendea ili adumishe upendo. Kama ni unene au wembamba  eleza! KISA CHA MWANAMKE  mwembamba akala akawa mnene – matokeo ni kuachwa.
-          Hatua ya pili:- WATOTO – elewa watoto sio sio lazima ila wanapokuwepo ni mbaraka ambao umeongezewa. Maana mbaraka wa kwanza ni kupata mke au mume na kumuita wangu wakati ni mali ya MUNGU.  Watoto wanaongezea furaha lakini upendo kwanza. ZABURI 127:3. Kisa cha mtu aliyeng’ang’ania kupata mtoto lakini hakupata kisha akamwacha mke wake matokeo alioa mke na kupata watoto watano – wote ni mang’aa yaani balaa. Leo 2005 anakiri mbele za watu kuwa alimlazimisha Mungu na anajutia kuwa na watoto maana wote hawana faida zaidi ya kumtia huzuni! Fedheha! Aibu tupu !
-          Hatua ya tatu:- KAZI.  Kazi inaongeza furaha kila mmoja anapowajibika kwa juhudi. Inaondoa umaskini kisha inaleta furaha. Mama fanya kazi usiwe golikipa. Utaimarisha upendo. Kila mmoja afanye sehemu yake.
-          Hatua ya nne:- MWONEKANO WA NJE – PHYSICAL APPEARANCE. Kosa la wanandoa wengi ni kuoa sura. Ni kosa la hatari. Upendo wa kweli hauangalii katika vitu hivyo bali katika tabia safi. Kama tabia ni mbaya basi hata sura ikiwa nzuri kiasi gani, itakuwa mbaya wakati chuki inapoingia. Kumbuka visura ni wengi na bado hawajazaliwa. KOLOSAI 3:12 – 14.
-          Hatua ya Tano:- MAWASILIANO. – Hakuna upendo feki utakaojenga nyumba. Lazima mawasiliano yawe yameunganishwa kila wakati. Kama hakuna mawasiliano ndani ya nyumba hakuna faida ya kuishi pamoja. Upendo wa kweli unapatikana kwa mfalme wa Amani – YESU KRISTO MWASISI WA NDOA. Adamu alipomuona hawa kwa mara ya kwanza aliwasiliaana naye kwa tabasamu na shukrani tele. Angalia Paulo asemacho katika Wakolosai 3:15 – hiyo ndiyo ndoa ya kweli. Haya hayatanonekana ikiwa mawasiliano yamekatika au kuvunjika. MAWASILIANO NI UFUNGUO WA UTAJIRI KATIKA NDOA. Iwe ni raisi wa  nchi  ndani hakuna maelewano basi nchi yote inayumba. Au hakimu mahakamani – sheria yote inapotea. Mchungaji – mahubiri na mafungu hayaji. Kisa cha rubani wa ndege.
-           
ISHARA ZA MAWASILIANO KUKATIKA NDANI YA NDOA: UTAJUAJE?
UPANDE WA MWANAMKE:- MITHALI 5:15 – 18, 20 – 21. MUHUBIRI 7: 26 – 28.
Usiombe wewe mwanamume kukatiwa mawasiliano na mwanamke hasa anapokuwa ameunganisha mahali Fulani huko nje; hata kama ni maskini kiasi gani huyu mtu huwezi kumtoa utapiga ua HATOKI MTU!
  • Maji ya kuoga ni baridi wakati alikuwa analeta ya moto halafu sababu nyingi.
  • Chakula cha baridi kwa madai alipika saa nyingi wewe ndiwe umechelewa.
  • Unapomwita anaitikia mmh! Eeh! Unasemaje? Au anakuja tu.
  • Kuwa na madai mengi ya kusahau – kufua, kupasi, chakula, maji ya kuoga, n.k.
  • Majibu ya mkato – makazi yote haya umeona mi msukule, mi kainjini au tractor.
  • Tabasamu na kicheko hakuna. Lakini akija mgeni atachangamkiwa mpaka …..
  • Kuwa na hasira za mara kwa mara yaani kununa unapokuja au unapomsemesha.
  • Kutokutulia nyumbani kila saa kwa mashoga – amepata tuition ya mafiga matatu.
  • Kutokupokea unaporudi hakuna tena – anajifanya kama vile hajakuona na kwenda ndani ama kutokusindikiza unapotaka kusafiri. Utabeba begi lako mwenyewe mpaka...
  • Kutokufua nguo zako ama kupasi nguo mpaka umkumbushe ama ufue mwenyewe.
  • Kuchelewa akienda sokoni ama bombani na pia kuchelewa kupika kwa wakati ili uende na njaa kazini ama katika shughuli zako.
  • Kukulaumu kwa mambo mengi hasa nguo zake, ama chakula ama fedha unazompa anadai kidogo.
  • Kuficha simu yake inapoita anakwenda mbali ili kupokea simu yake kukwepa mume wake asijue. Ishara ya karibu sana ni pale simu hiyo inapomuhusu mpenzi wake atashituka. Simu yake hataiweka chini na hataki uwe nayo.
  • Mwisho salamu hakupatii tena, anaanza kwa kubip kwa magoti kama ni msukuma… hatimaye kubip kwa magoti hakupo tena kama ni kupiga magoti linaondolewa kabisa.

UPANDE WA MWANAUME:- MITHALI 15:17.
Wanaume ndio wanaoongoza kukata mawasiliano haraka katika ndoa. Hasa asiporidhishwa na msiba wake wa maisha yaani tendo la ndoa. Ndoa nyingi zinaharibika kwa sababu ya mambo yanayoanzia chumbani. Hivyo wachungaji na viongozi wa jamii wamekuwa wanatatua matawi badala ya shina lenyewe yaani tendo la ndoa,. Tofauti ya mwanaume na mwanamke ni kuwa mwanaume anapokata MAWASILIANO LAZIMA AUNGE HARAKA KWENYE MTANDAO MWINGINE. MWANAMKE KAMA NI BUZZ 0741 ATAHAMIA 0717. Lakini mwanaume lazima awe kwenye line wakati wote yaani BUZZ basi ataenda vodacom na celtel. Hivyo anakuwa na mitandao mingi maana anafanyia kazi mahali ambapo hakuna network.
  • Tabasamu na kicheko hakuna – ni ndita tu. Hili ni jambo la kwanza kila unapopiga simu “ the mobile number you are calling is busier the present; may you try again later.” – Tabasamu imehamia mahali fulani.
  • Mambo yake ni siri tu – mshahara wake, viwanja, mipango, n.k. wewe unapewa taarifa tu maana wewe ni housegirl tu.
  • Vizawadi hakuna tena. – kisa cha maua kwangu.
  • Kuchelewa kurudi nyumbani – kutopenda kuketi nyumbani masaa ya jioni bali kwenda kwa mtu au vijiweni.
  • Kufokafoka ovyo kwa watoto na mke na hata kwa wanyama – kuku, mbwa, paka, n.k.
  • Kutokula nyumbani bali kwa mama ntilie/ hotelini – kisa cha mama ntilie na mzee wa kanisa.
  • Kisha anaanza kupokea simu nje kama ni ndani ama mbali na mahali ulipo. Atakuwa mkali unaposhika simu yake. Hasa unaposoma message zake.
  • Hakuna salaam tena; na hata ukimsalimia ataitikia kwa ndani tu.
  •  Majibu ya mkato; haswa anapoishiwa fedha – mi kabenki, sawa! Haya! Tayari! Eeh! Nitakwenda. Nitanunua. N.k.
  • Kutokuamini mke wako. Ndo unarudi? Kwanini umechelewa? MITHALI 14:15.
  • Kukuita kwa dharau – wee mamaa nanihi. We mwanamke. Hebu niitie huyo.
  • Kudharau kila kazi unayofanya hakuna pongezi wala shukrani.
  • Hakuna mazungumzo yanayofanyika mpaka mgeni anapoingia – yametoweka.
  • Kunung’unika kwa jambo moja kwa muda mrefu. Kukulaumu mara kwa mara.
  • Madai ya kuumwa mgongo kila siku – hakuna tendo la ndoa kama kawaida.
  • Zingatia kwa makini ndoa tajiri kupita zote Suleimani anasema ni ya maskini mmoja aliye na YESU: “kula mboga za majani na upendo ni bora, kuliko ng’ombe aliyenona na magomvi” Yesu unapomwalika hakika ndoa yako itakuwa na mibaraka na nyumba yako amani tele. Hakuna upungufu wa divai wala hakuna magonjwa wala balaa bali furaha na kicheko cha furaha tele! 

No comments:

Post a Comment

Nakuthamini

ikiwa kuna jambo lolote zuri lenye kuboresha au kufundisha usisite kuwasiliana nami. Blog hii ni kwa ajili yetu wote kutufundisha na kutuelekeza yatupasayo kutenda kwa maana wakati umekaribia ambapo yeye ajae anakuja na wala hatakawia. Nyosha mapito yako,tambua tabia yako kila mtafute Bwana maana anapatikana nawe ukimwita atakuitikia.