SEMINA: MAJUKUMU YA MWANAFAMILIA
(Masomo ya Kaya
na Familia, Makambi ya 2013: Mtayarishaji: Mkurugenzi wa Vijana, TU)
A.
UTANGULIZI: KWA
NINI SEMINA HII IFUNDISHWE KWA WANAFAMILIA?
Semina hii ni ya muhimu kwako
kwa sababu mbili kuu. Kwanza changamoto za kimahusiano zinazotokana na jamii
ilivyo kwa sasa zinakuhusu, maana huwezi kujiepusha na mambo ya kijamii. Pili changamoto za kifamilia
zimeathiri maisha ya kiroho ya walio wengi, hivyo kujikuta wakimpatia Mungu
nafasi ya pili badala ya nafasi ya kwanza. Huwezi kujiepusha na mambo ya kiroho
kisha ukafanikisha mambo ya kifamilia. Mambo ya kijamii na mambo ya kiroho
yanatakiwa kuunganishwa kwa ustadi ili mwanadanu apate sifa ya kumpendeza Mungu
na kuwapendeza wanadamu. Sababu hizi mbili zinafafanuliwa kwa kutumia vipengele
vifuatavyo:
Hoja
za kijamii
a. Hutuwezi kujiondoa katika masuala ya Kaya na kifamilia
1.
Kwa
kuzaliwa kila mtu huwa ni mtoto katika
familia ya wazazi wake.
2.
Kwa kuoa
au kuolewa mtu huanzisha familia yake wenyewe bila kutupilia mbali familia ya
wazazi wake.
3.
Familia
moja huunda ukoo, jamaa na jamuia tunamoishi.
4.
Maadili
ya familia moja huunganika na maadili ya familia nyingine na kuitwa maadili ya
jumuia.
5.
Itikadi,
mazoea na utamaduni wa jamuia
ni matokeo ya itikadi na
mazoea na utamaduni wa kaya/familia moja moja zikiwekwa pamoja.
6.
Kaya ndiyo muhimili unaoathiri familia na
jamii. Ni sahihi pia kusema kuwa
kaya ndiyo muhimili wa Taifa
lolote na muhimili wa Kanisa maana tunaiona jamii katika jicho la kaya moja
moja na athari zake.
b.
Kaya na Familia kama jicho la
Taifa
1.
Uaminifu
katika taifa mzizi wake uko katika uaminifu ndani ya familia
2.
Migogoro
ndani ya taifa hueleza migogoro ndani ya familia
3.
Ufisadi,
rushwa na dhuluma katika taifa hueleza ufisadi, rushwa na dhuluma katika
familia.
4.
Taifa
linapojaribiwa kusambaratika/kuvunjika ni taarifa kuwa familia zimetengana au
zimevunjika.
5.
Taifa
haliwezi kupenda vita endapo familia zilizo ndani yake hazipendi vita, maana
waathirika wa vita watakuwa ni wanafamilia.
c. Kaya na Familia kama jicho
la Kanisa
1.
Waumini
wa kanisa wanatoka katika kaya moja moja, ambao hutumika kama matofali ya
kujengea Kanisa.
2.
Ubora wa
maisha ya kaya/familia moja moja hutangaza ubora wa maisha ya Kanisa
3.
Unachokiona
ndani ya familia kitaonekana ndani ya Kanisa
4.
Kisichoonekana
ndani ya familia hakitaonekana ndani ya kanisa
d. Je ni nini kinachotokea katika Familia leo?
1.
Mtazamo
kuhusu ndoa unabadilika –kutoka kuwa
AGANO na kuwa MKATABA
2.
Mgogoro
katika majukumu ya wana ndoa. Yampasayo mume au mke yanapingwa kwa hoja za
kimaendeleo- haki sawa kwa wote.
3.
Msongo
unaotokana na masuala ya kifedha unazidi kuongezeka miongoni mwa wanafamilia.
4.
Kanuni
za ndoa zilizo heshimiwa kiafya zinakataliwa kwa kigezo cha mageuzi ya
kimaendeleo.
5.
Mzazi
kutokuwa na muda wa kukaa na mtoto anayehitaji malezi yake,(Parenting
inadequancy)
6.
Vurugu
na magomvi katika familia- mawasiliano kukatika
7.
Familia
kuvunjika na kubakia Kaya zilizojitenga
8.
Kasi
kubwa ya talaka inayochochea watoto kukosa maskani ya wazazi yanayoeleweka.
9.
Kubomoka
kwa mfumo wa kifamilia, kama matokeo ya ongezeko la watoto waliozaliwa nje ya ndoa.
10. Maisha ya kukata tamaa,
kutengana na hasira
11. Wazazi kuwatelekeza watoto
wao kwa sababu zozote wanazokuwa nazo.
12. Watoto kutowahudumia wazazi
wao kwa vigezo mbalimbali vikwemo wao kujiona ni wazazi
pia au kujilipiza kisasi kwa vile wao pia walitelekezwa katika makuzi
yao.
Hoja
za Kiroho
a) Kaya na Familia ni changamoto kwa Kanisa
1.
Kwa kuwa
nyumbani,(kaya), ndiko chimbuko la tabia, lugha, na mahusiano yote;
2.
Na kwa kuwa nyumbani,(kaya),kunamfuata mtu
kokote aendako, ikiwemo Kanisani;
3.
Kanisa
linalo jukumu maalumu la kuzisaidia kaya na familia ili tabia inayaotakiwa
kuonekana kanisani ianzie kuonekana nyumbani.
4.
Utaratibu
wa kanisa kupeleka huduma zake nyumbani katika kaya moja moja ni kanuni ya
kibiblia na haitakiwi kupuuzwa.
5.
Kabla ya
dhambi na baada ya dhambi, Mungu ameonyesha kujishughulisha na mtu mmoja mmoja
ndani ya familia, ijapokuwa wakati mwingine hutenda kwa kutumia familia
nzima,(Mwanzo 2:16,17; 3:8-19; 4:3-7).
b)
Changamoto za kifamilia zina
athari kwa makuzi ya kiroho.
Familia
ya kwanza kabisa, ya Adamu na Hawa, hutufundisha ubaya wa dhambi na matokeo
yake yasiyopendeza:
Ø
Rejea na
tafakari kisa cha Mwanzo 4:1-8, kumuhusu Kaini Habili na Adamu.
Ø
Wazazi kuwa
waanzilishi wa matatizo; watoto wakawa ni waathirika wa kwanza kwa
makosa ya wazazi wao.
Ø
Maneno yanayosemwa na ndugu
katika familia yanaweza kusikika kama mazuri kumbe yana mauaji ndani
yake,(mkakati wa Kaini).
Ø
Uaminifu
na utiifu kwa Mungu, (mfano wa Habili katika familia ya Adamu), waweza kuchochea mabaya dhidi ya
mhusika, yaliyotendwa na wenzake, bila Mungu kuingilia kati ili kuokoa maisha
yake.
Ø
Uhasama
miongoni mwa watoto wa Adamu,
uliochochea hasira hadi mauaji ulitokana na matendo ya kidini, yaliyosigana
katika msingi wa kiroho.
Ø
Migogoro
katika familia nyingi huchochewa na mitizamo au itikadi za kidini zilizo
tofauti miongoni mwa wanafamilia, na
hasa tendo la ibada.
Ø
Mungu
ameruhusu tendo la ibada liwe kiini cha pambano kuu. Je ibada yako inazingatia maagizo ya Mungu au maagizo yaliyo na msingi
wa kifamilia tu?
c)
Ujio wa Yesu wa mara ya
kwanza ulitanguliwa na mtayarishaji wa njia aliyeandaliwa toka nyumbani ndani
ya kaya na familia. Huyu ni Yohana Mbatizaji, (Math3:1-3).
Ø
Je yuko
mwanafamilia anayeandaliwa kwa ajili ya kumtengenezea Yesu njia ili awaokoe
watu kupitia utume wa familia yenu?
Ø
Kama
hayuko mwanafamilia kwa kusudi hilo, je familia nzima ina mpango gani wa
kumtambulisha Yesu kwa jamii iliyokosa maadili?
Ø
Ujumbe
wa Yohana mbatizaji, yaani Eliya aliyetabiriwa, ulianza kwa kupatanisha familia
kwanza,(Luka 1:13-19).
Ø
Ujio wa
Yesu wa mara ya pili utanguliwa na
ujumbe wa kupatanisha familia pia,(Malaki 4:5,6)
Ø
Ujumbe
wa mwisho kwa ulimwengu huanzia kwa familia kuisikia sauti ya Mungu. Hii ni kwa
sababu uovu huanzia kwa mtu mmoja mmoja ndani ya ndoa kwanza kisha ndani ya
familia.
Ø
Unabii
wa utimilifu wa kujirudia mahusiano ya aina hii umewekwa wazi na Kristo
mwenyewe katika Biblia. Rejea Math 24:36-41 juu ya uzoefu wa Nuhu, Lutu na
maadili ya zama hizi.
Nini kifanyike kusaidia changamoto hizi kwa
njia ya kanisa?
Programu
maalumu ya uamsho na matengenezo
yenye lengo la kuzipatanisha familia
kabla ya
ujio wa Yesu mara ya pili inatakiwa kuandaliwa na kila kanisa ili kufanikisha yafuatayo:
1.
Kuwafundisha
wanafamilia jinsi ya kuishi kama watu wanao wajibika kwanza kwa Mungu, pili kwa familia zao kila siku.
2.
Kuwasaidia
wanafamilia kupata uelewa wa jinsi ya kukabiliana
na changamoto za kimahusiano- mume na mke; mzazi na mtoto, n.k
3.
Kuzisaidia
familia jinsi ya kutumika kama vyombo vya kutangaza neema ya Mungu. Hii ni kwa
sababu maisha huanzishwa na Mungu na hukomeshwa na Mungu. Kuyajua maagizo ya
Mungu ni muhimu maishani.
4.
Ikumbukwe
kuwa: ‘familia moja iliyo na nidhamu na
utaratibu mzuri, huwa na mvuto wa nguvu
zaidi kwa niaba ya ukristo (kuuelezea ukristo) kuliko mahubiri yote yanayoweza
kuhubiriwa’, (Adventist Home uk 32).
5.
Ikumbukwe
kuwa: ”Kuwa sehemu ya familia ni rahisi sana; kudumisha uhusiano wa kifamilia
ni zoezi gumu. Kuishi kwa furaha katika familia uliyomo bila msaada wa Mungu,
inaaminika kuwa ni sanaa inayofikirika.
6.
Endapo kijana hakupewa malezi mazuri na wazazi
wake na hivyo hali hiyo kuchangia tabia
mbaya anayoidumisha, hilo halitakuwa ni udhuru mbele za Mungu, maana ni jukumu lake kusahihisha tabia
iliyoharibika maishani mwake bila kutoa udhuru wa kutolelewa vizuri. Hivyo
wahusika na malezi ya vijana ni wote: Wazazi, Kanisa kupitia Idara husika, na Vijana wenyewe. Hoja ni, “Je
unafanya nini kutimiza wajibu wako”? Tambua wajibu wako na uutimize.
B. UWAJIBIKAJI WA KILA MWANAFAMILIA
Kila mwanafamilia
anao uwajibikaji anaodaiwa kila siku ili
kuboresha mahusiano ya kifamilia ndani
ya familia yake na katika jamii aishimo. Tukiyaunganisha mashauri ya Mtume
Paulo anayoyatoa katika 1Timotheo 5 na Waefeso 5 na 6, tunapata uwajibikaji wa
madaraja manne, kila daraja na
uwajibikaji unaolipasa. Tutafafanua uwajibikaji wa kila daraja miongoni mwa
madaraja manne yafuatayo:
1.
Mwana familia kama Mtoto na majukumu yake
2.
Mwanafamilia
kama Mzazi na majukumu yake
3.
Mwanafamilia
kama Mwenzi na majukumu yake
4.
Familia
kama kiungo cha jamii na majukumu yake
C. MWANA FAMILIA KAMA MTOTO (MAJUKUMU YAKE)
1. Je Mtoto ni nani
na ni lini mtu hukoma kuitwa mtoto?
Maana ya neno
“mtoto” kibiblia huvuka ile ya kikamusi. Kikamusi mtoto ni mtu mwenye miaka
chini ya 18 ya umri. Kibiblia mtoto ni yule anayejielewa kuwa anao wazazi
anaowaita “Baba” au “ Mama” kimahusiano, anaotegemewa awahudumie kwa heshima
zote,(Kutoka 20:12; Waefeso 6:1-3; 1Timotheo 5:1-4). Katika mtizamo huu utoto
wa kifamilia hukoma wazazi wanapoisha kwa kufariki.
2. Majukumu binafsi yampasayo mtoto mwenyewe?
1)
Mtoto
analo jukumu la kutafuta kujua maana ya maisha na kuishi.
2)
Kuwepo
duniani kisha mtu asijishughulishe kujua imetokeaje akawepo hapo alipo na
makusudi yake, ni udhihirisho wa kutokuwajibika.
3)
Kujitambua
yeye ni nani na kusudi lake ni nini huwa miongoni mwa masomo yaliyo elimu ya msingi katika uwajibikaji
wake katika kuishi. Rejea Zaburi 139:13,14.
4)
Kutokuuliza
anavyotakiwa kufanya katika kutimiza kusudi la maisha hudhihirisha
kutokuwajibika.
3. Majukumu ya mtoto kwa mzazi
1)
Agenda
kubwa huwa ni kuwalipa wazazi wao kihuduma, (1Timotheo 5:1-4)
2)
Jukumu
la kuwahudumia wazazi huwa halitolewi udhuru kimahusiano. Mjane hategemewi
kutoa udhuru kwa kutokuwahudumia wazazi wake kigezo kikiwa kuwahudumia watoto
wake,(1Timotheo 5:1-5). Unapokuwa ni mtoto na ukawa mzazi pia majukumu huongezeka.
3)
Kwa
kuwa mzazi alimlea utotoni, mtoto naye anategemewa amlipe mzazi kwa malezi
aliyopewa,(1Timotheo 5:4), hasa pale nguvu zinapokuwa zinazidi kumupungua.
4)
Jukumu
maalumu la mtoto analolisema Mfalme Sulemani ni “kumfurahisha mzazi wake”( Mithali 23:24, 25). Kumfurahisha mzazi ni
tendo endelevu la kila siku maishani, linalodhihirishwa na kumpa heshima na
utii anaositahili kama mzazi,(Kutoka 20:12; Waefeso 6:1-3).
5)
Miongoni
mwa matendo yaletayo laana kwa watoto limo hili la kumdharau mzazi wake, (Kumb/Torati
27:16). Kauli hizi zinasisitiza kuwajali wazazi na kuwahudumia muda wote.
4. Majukumu ya mtoto kwa wanafamilia na kwa jamii
1)
Yesu
ndiye kielelezo cha makuzi na matendo yote ya
maisha.
2)
Katika
Luka 2:52 tunaambiwa katika makuzi yake alidumu kumpendeza Mungu na kuwapendeza
wanadamu. Wanadamu wanaosemwa hapa sio ndugu zake tu bali ni wote.
3)
Katika
1Timotheo 5:1-3 Mtume Paulo anawaanza vijana na watoto kudhihirisha maisha
yenye upendo na huduma kwa wengine wasiokuwa ni ndugu. Asema,” Mzee usimkee,
bali umwonye kama baba; na vijana kama ndugu; wanawake wazee kama mama;
wanawake vijana kama ndugu wa kike; katika usafi wote. Uwaheshimu wajane walio
wajane kweli kweli”. Hii ni jamii
inayoongelewa hapa.
4)
Katika
Waraka wa kwanza wa Yohana sura ya pili mafungu ya saba hadi kumi na moja
tunaambiwa, ukiishi kwa kumuchukia ndugu yako unakuwa unaishi gizani wala si
nuruni tena unakuwa hujui utokako na uendako. Maisha yetu ni lazima yawe na
faida kwetu na kwa wengine.
5)
Katika
1Yohana 4:20 tunaambiwa kwamba, “Mtu akisema, Nampenda Mungu, naye anamchukia
ndugu yake, ni mwongo; kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye anamwona, hawezi
kumpenda Mungu ambaye hakumwona. Na amri hii tumepewa na yeye, ya kwamba yeye
ampendaye Mungu, ampende na ndugu yake.”
6)
Unapokuwa
ni mtoto miongoni mwa wanafamilia ya wazazi wako, majukumu huongezeka ili
kuwahudumia wazazi, ndugu na jamii.
D. MAJUKUMU YA MWANAFAMILIA KAMA MZAZI
1. Mzazi ni nani, na ni lini mtu hukoma kuwa mzazi?
1)
Mzazi
ni yeyote yule aliyeshiriki tendo la kufanya mtoto azaliwe.
2)
Kwa
mujibu wa maana hii ya mzazi, wapo wazazi wanaozaa kihalali na wanaozaa
kiharamu.
3)
Iwayo
yote, mtu hukoma kuwa mzazi anapkuwa hana watoto wa kulea, au hana watu
wanaomwita mzazi.
2. Majukumu ya Mzazi kwa Mtoto wake
1)
Watoto
wawe wamezaliwa kihalali au kiharamu wote huwa ni watoto wa mzazi, na uwajibikaji wa mzazi
kwao unafanana.
2)
1Timotheo
5:7,8 inataja jukumu mojawapo la mzazi kuwa ni utunzaji wa watoto wake.
Tunapozaa na tukakwepa kutunza kunakodhihirishwa na kujali kisha
tukimbilie kwa Mungu, hata ibada yetu kwa Mungu huwa haikubaliwi.
3)
Mithali
22:6 inataja jukumu jingine la malezi. Kulea
kunakotajwa hapa kunahusisha mafundisho, ambayo hayategemewi kuachwa hat
atakapokuwa mzee.
4)
Tunapozaa
na kuwa mbali na watoto huwa vigumu kutekeleza malezi yawapasayo. Katika Kumb/Torati
6:4-9 tunaelezwa mazingira tunamolelea watoto: tutembeapo njiani, tuketipo
katika nyumba zetu, tulalapo, tuondokapo, tena kwamba ni agizo la Bwana
kuwafundisha watoto kwa bidii.
5)
Kwa
kifupi majukumu ya mzazi kwa mtoto ni ya aina 6 hivi: Kumfundisha, (Teach),
Kumwelekeza, (Train), Kumhudumia katika mahitaji ya maisha, (Provide),
Kumuadibisha, (Nurture), Kumtiisha,(control), na Kumpenda, kumwonyesha upendo), (to love).
Kila moja katika haya 6 ni mada inayohitaji mzazi ajifunze jinsi ya kuitekeleza
ipasavyo.
3. Changamoto za majukumu ya kuwa mzazi na jinsi ya
kuzikabili
1)
Mtoto
anataka muda wa kukaa na kufunzwa na mzazi, wakati mzazi anadhani anataka muda
wa kumtafutia mtoto mahitaji.
2)
Kutokukaa
na mtoto nyumbani kwa muda wa kutosha ni kushindwa kumfundisha majukumu
yafanyikayo nyumbani, hivyo kushindwa kumuandaa kuwa msimamizi wa shughuli za
nyumbani kwake anapokuwa mkubwa.
3)
Tabia na mazoea yote hujengwa katika umri mdogo
usiozidi miaka mitano, na hasa ule wa miaka miwili kurudi chini. Kumweka mtoto
mbali na mzazi katika kipindi hicho ni kunjengea mazingira yaliyomunyima ujenzi
wa tabia au njia impasayo.
4)
Kuwa
mtoto kisha uwe mzazi na uwe mwanafamilia utakiwaye kutumika kama ndugu kwa
wenzako kunagharimu kuoanisha muda na uwezeshaji.
5)
Kuhangaika
ili kutoa huduma za kimwili kwa watoto na hapo hapo uhakikishe huduma za kiroho
hazikupungua kwa watoto ndipo udhihirisho wa mzazi anatunza walio wake.
6)
Kitendo
cha kuwapeleka watoto wadogo katika shule za bweni ili wapate mzazi mwingine
huko ni kukataa jukumu la kulea ukabakiza la kuwa mzazi.
7)
Kutokuwashirikisha
watoto malezi ya kiroho kwa kwenda nao katika mikutano ya kidini na kuwahimiza
kuishiriki, na kuhakikisha mambo wanayojifunza ni kukosa muda wa kuwafanya
watoto wamjue Mungu na kumpenda. Wanaposhindwa kumjua Mungu na kumpenda
hawatampenda mzazi kama alivyotazamia hapo wawapo watu wazima.
8)
Kuwazuia
watoto wasishiriki katika progarmu za Idara ya vijana zenye lengo la kumsaidia
mzazi kuwapatia watoto malezi ya kiroho na kuwaandaa kwa uongozi wa kanisa, ni
kuwanyima fursa ya kulipenda kanisa na kumtumikia Mungu kwa njia ya kanisa.
9)
Tunapoamua
kusomesha watoto wetu katika shule zisizo za kanisa letu kwa vigezo vyo vyote
vile, huwa ni ukubali kuwa makanisa hayo yana elimu na malezi bora kuliko ya
kanisa letu. Watakapoharibika kitabia mzazi atabebeshwa hatia ya mtoto maana amemtengenezea mazingira ya
malezi yaliyomuathiri mtoto.
10) Ikumbukwe kuwa
sio rahisi kuondoa madhara ya elimu mbovu aliyopewa mtoto kwa masaa 9 kutwa kwa
kutumia dakika 20 za maombi ya nyumbani wakati somo linalojadiliwa halikumlenga
yey bali watu wazima.
11) Haya yote
yangetupatia hadhali kuwa tunatakiwa kurekebisha ratiba za utendaji wetu ili
kuwa na muda wa kutosha kusadia tabia za watoto wetu ili wapate kuokolewa.
E.
MAJUKUMUYA MWANAFAMILIA KAMA MWENZI (WANANDOA)
1. Mume na Mke katika
ndoa wanatambulikaje?
1)
Kwa
mujibu wa sheria ya ndoa ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, mume na mke
hutambulika kwa vigezo kadhaa, miongoni mwake vikiwemo: kuwa na cheti cha ndoa;
kuonekana wakiishii ndani ya chumba kimoja kwa kipindi kisichopungua miezi sita
hata kama hawana cheti cha ndoa.
2)
Kibiblia
mume na mke hutambulika kwa kuwa uchi wote wawili, kama hatua ya kuwa mwili
mmoja, (Mwanzo 2:24,25)
2.
Mume na Mke
katika ndoa majukumu yao ya msingi ni yapi?
Kusudi la kuwepo
mke ni ili awe mwenzi kwa mume, ambaye ni msaidizi wa kufanana naye, (2:18). Je
ni nini kinachodhihirisha utendaji wa kuwa mwezi au msaidizi wa kufanana na
mwenzake?
1)
Kuishi
maisha ya kuambatana wote wawili, (Mwanzo 2:24)
2)
Kuyachanganya
ama kayunganisha maisha ya wawili kuwa kitu kimoja,(Kutay/Njia-1 uk.147)
3)
Kuitumikia
furaha ya mwenziwe kwa kufurahishana kila mmoja,(Kutay/ Njia-1 uk.143.
4)
Ili
majukumu hayo matatu yatekeleze, kunahitajika wasifu au vigezo vingine
vinavyoendana ili kuboresha mahusiano hayo. Vigezo hivyo vinaorodheshwa kuanzia
no 5 kuendelea.
5)
Anayejiandaa
kuwa mume au kuwa mke inabidi ajifunze jinsi ya kujitawala na jinsi ya
kuwatendea wengine, (Kutayarisha Njia- 1 uk.145).
6)
Kuunganisha
maisha ya wawili kuwa kitu kimoja kunamhitaji kila mmoja kuongeza uvumilivu kwa
kutumia uvumilivu,(Kutayarisha Njia-1 uk.147).
7)
Mume
aishi kwa kumpenda mkewe kama Kristo anavyolipenda Kanisa, kwa lengo la
kulisafisha, akilenga kuwa mwokozi wa mwili badala ya kuunajisi, Waef.5:22-28).
8)
Mke
aishi kwa kumtii mumewe katika kila jambo kama Kanisa limtiivyo Kristo,
(Waefeso 5:22-24).
9)
Majukumu
kuanzia no 5-8 yanawaelekeza wanandoa kutafuta kujua mapenzi ya Mungu
yanayofanikishwa na mahusiano ya kindoa. Mashauri ya kuishi kwayo katika ndoa
sio yale yatokanyao na mila zetu bali ni yale yatokanayo na Biblia
inavyoelekeza.
10) Ni katika
muktadha huu tunapopata jukumu la nyongeza la wanandoa kuwa na muda wa pamoja
wa kumwomba Mungu ili awaoneshe watakiwacho kufanya na jinsi ya kukifanya ili
kumpendeza Mungu. Changamoto kubwa ya mwanadamu ni,”Kufanya kitakiwacho, kwa
wakati utakiwao, na kwa namna itakiwayo”, (Christian Service, EG. White)
F. MAJUKUMU YA FAMILIA KATIKA JAMII
1. Familia inayo huduma gani kwa Familia jirani?
Kila mkristo
anatgemewa aishi katika jamii akidhihirisha uwajibikaji wa aina mbili, yani
kutumika kama chumvi na kama nuru, (Math. 5:13-16). Ufanunuzi wa uwajibikaji
huu unaelezwa katika aya zinazofuata.
1)
Familia
iishi kwa namna ambayo italeta radha ya kimadili ikilenga familia jirani
zijifunze maadili yampendezayo Mungu kutoka kwa familia hiyo.
2)
Familia
iishi kwa kuzuia uozo wa kitabia kwa kukemea matendo maovu yanayofanyika katika
ujirani wake ili kziambukizza familia zingine kufanya yale yampendezayo Mungu.
3)
Familia
iishi kama nuru inayoonesha njia kwa wasioijua njia ya wema na haki na kweli
ikihimiza familia zingine kufuata kielelezo chake.
4)
Ili
kufanikisha uwajibikaji wa aina hii familia haitegemewi iishi katika mazingira
ya kujitenga na jamii kwa lengo la kuepuka uovu na dhambi. Inategemewa kuishi
kwa kuchangamana na jamii bila kuchanganyika, (Yohana 17:14-18; 1Wakorintho
5:9-13).
5)
Kuishi
kwa kuchangamana na jamii ni kulia na wanaolia, kufurahi na wanaofurahi,
kuhuzunika na wanohuzumika kwa kuwasaidia katika magumu ynayowaumiza, kisha
kuwaalika kumwamini na kumtii Mungu unayeishi kwa kumtumikia.
2. Maswali muhimu ya kujiuliza
1)
Je
familia yako inazo familia rafiki zisizo za waumini wenzako kwa ajili ya
uinjilisti?
3)
Kama
majibu ya maswali haya ni hapana, unahitajika kufanya matengenezo kifamilia.
No comments:
Post a Comment